Wednesday, February 19, 2014

Watatu Waombewa Uhamisho Wa Kimataifa Wachezaji watatu wanaocheza mpira wa miguu nchini Tanzania wameombewa Hati ya

Wachezaji watatu wanaocheza mpira wa miguu nchini Tanzania wameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ili wakacheze katika nchi za Thailand na Ujerumani.

Mchezaji Khamis Mroki Jamal aliyekuwa na timu ya Daraja la Kwanza ya Polisi Dar es Salaam ameombewa ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Thailand (FAT) ili akajiunge na Kabinburi ya nchini humo.

Said Ali Nassor aliyekuwa akichezea FC Turkey ya Zanzibar na Samuel Chuonyo wameombewa na ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) kwa ajili ya kujiunga na klabu ya VfB Eichstatt.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo ridhaa ya klabu zao za hapa Tanzania itatoa ITC hizo.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Watano Walalamikiwa Kamati Ya Maadili Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewalalamikia wana familia watano wa mpira

Watano Walalamikiwa Kamati Ya Maadili Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewalalamikia wana familia watano wa mpira

Saturday, February 15, 2014

YANGA YAFUZU HATUA YA PILI, YAICHAPA KOMOROZINE de DOMONI 5 -2, NGASA ATUPIA HAT-TRICK


Mrisho Ngasa akipokea zawadi ya mpira kutoka kwa mwamuzi wa mchezo wa leo kutoka Sychelles Allister Barra wa kufuatia kufunga mabao matatu (hat-trick)
Wawakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Young Africans leo imeweza kufuzu raundi ya pili ya mashindano hayo kufuatia kuibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya wenyeji timu ya Komorozine de Domoni katika mchezo uliofanyika jioni ya leo katika dimba la Uwanja wa Sheikh Said Ibrahim Mitsamihuli.
Ikicheza mbele ya Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw. Chabaka Kilumanga Young Africans imefanikiwa kufuzu hatua ya pili ya Mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika kwa jumla ya mabao 12- 2, kufutaia ushindi wa mabao 7-0 katika mchezo wa awali uliofanyika jijini Dar es salaam huku Mrisho Ngasa akifunga "Hat-trick" katika michezo yote miwili.
Komorozine de Domoni ikicheza mbele ya Gavana wa jimbo lao la Anjuani iliuanza mchezo kwa kasi kwa lengo la kusaka bao la mapema ili kuwapa nguvu washangiliaji wao amabo walikuja kuipa sapoti timu hiyo.
Hamis Kiiza aliipatia Young Africans bao la kwanza dakika ya 13 ya mchezo kufuatia kuitumia vizuri krosi ya mlinzi wa kushoto Oscar Joshua aliyepanda kuongeza nguvu mashambulizi na pasi yake kumkuta Kiiza ambaye aliukwamisha mpira wavuni bila ajizi.
Dakika ya 22 ya mchezo, Mrisho Ngasa aliwainua mashabiki wa Young Africans vitini kufuatia kuifungia timu yake bao la pili kufuatia migongeo mizuri ya Haruna Niyonzima na Didier Kavumbagu.
Saimon Msuva aliipatia Young Africans bao tatu kufuatia kufanya shambulizi langoni mwa timu ya Komorozine de Domoni baada ya pasi za viungo Athuman idd, Haruna Niyonzima na Mrisho Ngasa kumkuta mfungaji ambaye hakufanya makosa.
Dakika ya 41 ya mchezo makosa ya mpira ulioptezwa na Hamis Kiziza yaliwapelekea Komorozine de Domoni kijipatia bao la kwanza baada ya mshmabuliaji wao kumtoka Oscar Joshua na kupiga krosi iliyomkuta mfungaji.
Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika, Komorozine de Domoni 1 - 3 Young Africans.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko ambapo Young Africans iliwaingiza Frank Domayo, Hassan Dilunga na Said Bahanuzi waliochukua nafasi za Athuman Idd, Saimon Msuva na Didier Kavumbagu mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mashambulizi.
Dakika ya 77 Korozine de Domoni walijipatia bao la pili kufuatia makosa ya kiungo Hassan Dilunga baada ya mpira alipoteza kunaswa na msahmbuliaji wa Komorozine na kuwazidi ujanja walinzi wa Young Africans na kuukwamisha mpira wavuni.
Mrisho Ngasa aliipatia Young Africans bao la nne dakika ya 87 ya mchezo kufuatia Said Bahanuzi kuwatoka walinzi wa Komorozine na kupiga krosi iliyomkuta Ngasa na kuukwamisha mpira wavuni kwa kifua.
Dakika ya 90 ya mchezo Mrisho Ngasa aliendelea kuwapa furaha tena washabiki wa Young Africans waliojitokeza uwanjani leo kuishangilia timu yao baada ya kuipatia timu yake bao la tano na la ushindi kwa kichwa baada ya kuitendea vyema krosi ya kiungo Haruna Niyonzima.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Komorozine de Domoni 2 - 5 Young Africans.
Mara baada ya mchezo mwamuzi wa mchezo wa leo Allister Barra alimkabidhi mpira mshambuliaji Mrisho Ngasa kufuatia kufunga mabao 3 peke yake (hat-trick) katika mchezo wa leo.
Baadhi ya watanzania walijitokeza kuishangilia timu yao ya Young Africans wakiongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Comoro Chibaka Kilumanga  walifurahishwa na ushindi huo na kusema wamefarijika na timu yao kwa kushinda mchezo wa leo na kusema wanaitakia kila la kheri katika michezo inayofuata.
Kesho mchana Msafara wa Young Africans umealikwa chakula cha mchana nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw.Ckibaka Kilumanaga  na siku ya jumatatu kikosi kitaanza safari ya kurejea nchini majira ya saa 6 mchana kwa shirika la ndege Precision Air.
Young Africans: 1.Dida, 2.Twite, 3.Oscar, 4.Cannavaro, 5.Yondani, 6.Chuji/Dilunga, 7.Msuva/Domayo, 8.Niyonzima, 9.Didier/Bahanuzi, 10.Ngasa, Kiiza

YANGA KUWAVAA KOMOROZINE de DOMONI LEO

Young Africans leo baadaye itashuka dimbani kucheza mchezo wa marudiano dhidi ya timu ya Komorozine de Domoni ya Anjuan Visiwa vya Comoro katika mchezo wa Klabu Bingwa Barani Afrika utakaofanyika mji wa Mitsamihuli kwenye uwanja wa Sheikh Said Mohamed International kuanzia majira ya 9 kamili mchana kwa saa za Afrika Mashariki. 

Mara baada ya juzi jioni kufanya mazoezi mepesi katika uwanja mdogo wa hotel ya Retaj, jana kikosi cha Young Africans kimeweza kufanya mazoezi asubuhi majira ya saa 5 ausbuhi katika Uwanja wa Sheikh Said kwa ajili ya kuuzoea tayari kwa ajili ya mchezo wa leo.

Kocha mkuu wa Young Africans Hans Van der Pluijm amesema anashukuru kikosi chake kipo vizuri kuelekea mchezo huo na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja hivyo anapata fursa ya kuchagua amtumie nani katika mchezo huo.

Akiongelea wapinzani timu ya Komorozine de Domoni amesema hawajaidharaua mechi ya leo kama watu wengi wanavyofikiria, kikubwa amewaandaa vijana wake waeze kufanya vizuri na kupata ushindi, "Kwangu mie hakuna mechi ndogo wala mchezo wa kirafiki" alisema Hans.

Young Africans itashuka dimbani kucheza mchezo huo wa marudiano ikiwa na kumbukumbu nzuri ya ushindi wa mabao 7-0 iliyoupata katika mchezo wa awali uliofanyika jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.

OKWI RUKSA YANGA

Mshambuliaji wa kimataifa wa timu ya Taifa Uganda na klabu ya Young Africans Emmanuel Arnold Okwi leo ameruhiswa ramsi kuanza kuitumikia timu yake katika michezo ya Ligi Kuu na Mashindano ya klabu Bingwa Barani Afrika kufuatia shirikisho la soka nchini TFF kuiandikia barua klabu ya Young Africans.

Okwi ambaye alisajiliw aa Young Africans mwishoni mwa mwaka jana na kucheza michezo ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya, alisimamishwa na Shirikisho la Soka la Nchini TFF wakati wakisubiria kupata udhibitisho wa usajili wake kutoka FIFA.
Mara baada ya barua hiyo, Okwi anatarajiwa kuungana na wenzake mwishoni mwa wiki mara timu itakaporejea kutoka Visiwa vya Comoro na ataanza kuonekana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Ruvu Shooting siku ya jumamosi Februari 22 mwaka huu.
Uongozi wa Young Africans unawashukuru wanachama, wapenzi na wadau kwa ujumla kwa kuwa wavumilivu wakati wa suala na hili na hatimaye limepatiwa ufumbuzi.

 www.youngafricans.co.tz

Magath in for Meulensteen at Fulham

Magath in for Meulensteen at FulhamFulham have taken drastic action in their bid to beat relegation by sacking Rene Meulensteen and appointing Felix Magath as first-team manager.
Former Manchester United coach Meulensteen was appointed head coach under Martin Jol, only to take control of first-team duties on 1 December following his compartiot's sacking.
However, with the bottom-placed west Londoners four points adrift of Premier League safety, chairman Shahid Khan has wielded the axe again.
Magath has been installed as first-team manager on an 18-month contract, with Meulensteen confirming his exit from the club despite the club statement not mentioning his name.
German manager Magath arrives at Craven Cottage with an impressive CV, having led Bayern Munich to successive Bundesliga titles in 2005 and 2006, before achieving the same feat with Wolfsburg in 2009.
Commenting on the decision, chairman Khan told the club's official website: "I am very happy to welcome Felix Magath to Fulham Football Club.
"Felix is an accomplished manager with multiple honours in the Bundesliga and a hunger to replicate his success with Fulham in the Barclays Premier League.
"I'm especially impressed with the reputation Felix has for coming into clubs at difficult times, often late in the season, and lifting them to their potential and beyond.
"Felix knows that is precisely the task awaiting him at Fulham, and he made it abundantly clear that he wants and is ready for the opportunity.
"Our club has shown promise in recent matches, but the fact is we have not won a league match since 1 January.
"Given our form, we can no longer merely hope that our fortunes will finally turn. And with 12 matches remaining and at least four points separating us from safety, we certainly can no longer post empty results. Action was required.
"[Chief executive] Alistair Mackintosh did a wonderful job during the January transfer window to improve our club.
"This week, Alistair recommended Felix, with his history of producing results for clubs with similar challenges as ours, as the new manager of Fulham.
"Alistair's recommendation received my complete approval and Felix has my unequivocal support."
While Fulham are bottom of the Premier League and four points adrift of safety, the decision to sack Meulensteen with only 12 matches remaining has taken the football world by surprise.
Last Sunday the Dutchman led the Whites to a 2-2 draw at Manchester United and on Wednesday his side put in an impressive performance against Liverpool, only for the league's in-form side to win 3-2 thanks to a stoppage-time penalty.
Meulensteen was informed of the decision by chief executive Alistair Mackintosh and believes the decision to press the "panic button" was wrong.
"I am very, very surprised, very disappointed, very frustrated as well, because the job that I stepped into was one that took me by surprise from the start, because that was not anticipated with Martin Jol leaving and obviously you then have to step into situation which is not the best," he told BBC Radio 5 Live.
"You need to try and make things better as soon as you can, but you're playing with a deck of cards that are not yours.
"I haven't really been given any time to make that work. I thought the performance against Manchester United and Liverpool were very, very good and it was unfortunate that we did not pick up the points that we deserved.
"Twelve games to go, plenty of points to play for and I'm sure we would have turned it around.
"I've not been told anything. I knew the owners were freaking out and panicking about the fact that Fulham could get relegated, but they've had that sort of attitude already ten games back.
"They've hit the panic button on emotions of fear, but hey-ho, that's what happens in football. It's not always fair."

Applauding the enemy

Football is a team game, of course, but every now and again it can seem like an individual sport. Few things stir a crowd like the sight of a player in peak form taking a match by the scruff of the neck, as proved by the likes of Ronaldo, Alessandro Del Piero, Ronaldinho and Alfredo Di Stefano down the years. Each of those legendary names left such a searing imprint on at least one game during their careers that they were feted like heroes as they left the pitch, with even opposition fans springing from their seats to applaud. FIFA.com now looks back at some of football's most memorable standing ovations.

Given the sheer intensity of the rivalry between Real Madrid and Barcelona, it might be difficult to believe that any one player could unite supporters on both sides of the divide. That, however, is precisely what Laurie Cunningham achieved during the 1979/80 season. The first Englishman to represent Los Merengues, Cunningham put in a stunning performance at the Camp Nou as the capital club clinched a 2-0 victory – and the locals were so moved by his display that they rose in unison as he departed the field.

It was a gesture the Santiago Bernabeu faithful have since repeated twice, first lauding an opposition talent a mere three years later. On 26 June 1983, the iconic venue was playing host to the return leg in the final of the Copa de la Liga, Spain's short-lived second knockout competition. With 57 minutes gone, Barcelona were leading 1-0 and a certain Diego Maradona was about to make things worse for the hosts, the Argentinian forward setting off on a mazy run that ended with the ball in the Madrid net. Both sets of supporters jumped up in sheer admiration – just as they did again in 2005 when Maradona's fellow South American No10, Ronaldinho, left his mark on another Clasico joust. The Brazilian danced through the right side of Madrid's defence before slotting past Iker Casillas and he bewildered the Merengues' rearguard moments later to round off a 3-0 win that even the home fans felt obliged to acclaim.
Indeed, it would be fair to say that the Santiago Bernabeu crowd are particularly quick to recognise when their heroes have been outplayed. They had already been stirred to a standing ovation in 1952, when Alfredo di Stefano showed off his skills for Colombian outfit Millonarios during a tournament to celebrate Madrid's 50th anniversary. Di Stefano helped himself to a double that day as his club triumphed 4-2, and the home fans liked what they saw. They would get to see much more of it too as the gifted forward soon signed for the Spanish giants, spending 11 trophy-laden years at the club. Dutch midfielder Gerrie Muhren never joined Madrid, in contrast, but he too brought 80,000 spectators to their feet at the Santiago Bernabeu, courtesy of a sublime display and a superb goal that propelled Ajax through to the 1973 European Champion Clubs' Cup showpiece.
Most recently, the Madrid faithful showed their appreciation for a rival player when Juventus paid a visit on 5 November 2008. The night belonged to Alessandro Del Piero, who helped himself to a pair of goals to leave the home side reeling in a UEFA Champions League group stage encounter. "Throughout my career, I have been shown many demonstrations of affection," Il Pinturicchio later explained. "But above all I remember two moments: the homage I received during my last game in Turin and the applause at the Bernabeu in 2008. To receive a standing ovation in such a temple of football is just priceless."
Applauding the enemy 
I remember when they substituted me in the second half, I left the field to an ovation from the fans. It was amazing
 
Ronaldo, former Brazil forward on his Old Trafford ovation


One player who could no doubt attest to that is Ronaldo, who had Old Trafford eating out of his hand in April 2003. Leading the line for Madrid, the Brazilian striker stunned Manchester United with a hat-trick that steered his side into the Champions League semi-finals, Los Blancos emerging 6-5 victors on aggregate. Despite the bitter pain of their imminent exit, the United fans duly paid their respects when the match winner was replaced by Santiago Solari on 67 minutes. "It was a magical night, just incredible," O Fenomeno told FIFA.com. "We had a great football match and the fans appreciated my performance. I remember when they substituted me in the second half, I left the field to an ovation from the fans. It was amazing."
At Arsenal, meanwhile, supporters tend to reserve their moments of praise for returning heroes – as Eduardo found in 2010. The Croatian marksman may have spent just three years with the Gunners, but he clearly left a huge number of admirers, the Emirates crowd standing as one to salute his consolation goal for Shakhtar Donetsk during a Champions League group stage win for the hosts. "I felt like I was still playing for Arsenal," he revealed afterwards, citing a sentiment that Thierry Henry must have experienced before him in the 2009/10 campaign. Returning to familiar ground for a Champions League quarter-final tie between Arsenal and Barcelona, the French striker received a rapturous welcome when he was brought on for Zlatan Ibrahimovic.
The Sweden captain is no stranger to ovations behind enemy lines either, particularly since he packed his bags for Paris Saint-Germain. Scorer of four wonderful goals away against Anderlecht during a Champions League group stage outing in October last year, Ibrahimovic walked off the pitch to a clamour of cheers – and four weeks later in Brest he was given the same treatment. This time, he had plundered a treble in a round of 64 Coupe de France tie, and he left Brittany with the applause of the sparse home crowd ringing in his ears. "The standing ovation when I went off? It wasn't difficult because there were 500 people in the ground," he said after the game. "But I'm very happy if people are happy."
Long before Ibrahimovic started getting into the habit, Brazil legend Pele was also parading a brand of genius that even rival supporters felt inspired to praise. No less a figure than the King of Sweden fell under his spell, in fact. "It was impossible not to applaud Pele's brilliance," enthused Gustaf VI Adolf after the host nation lost the 1958 FIFA World Cup™ final to A Seleção and their teenage phenomenon. O Rei was regularly honoured by opposition fans, and not least when he hit the target against Fluminense in 1961 after dribbling the ball past six opponents – a feat that sparked such delirium it took nearly two minutes for the match to resume.
Current Brazil star Neymar cannot point to the same trophy haul as his illustrious predecessor, but the two players have more than a little in common all the same. For a start, the Barcelona forward was playing for Pele's old club Santos when he brought down the house with a hat-trick away against the Cruzeiro in 2012. "I'm so emotional that I could cry," he told reporters after the final whistle.

In emotional terms, surely few moments can rival the closing stages of the Catalan derby between Espanyol and Barcelona on 12 December 2010, however. With 86 minutes gone, Barça coach Pep Guardiola opted to make one final substitution and brought off Andres Iniesta, the midfielder leaving the Estadi Cornellà-El Prat turf to a stirring reception from all four corners of the ground. A few months earlier, the Blaugrana stalwart had dedicated his winning goal in the World Cup final to Dani Jarque, the former Espanyol defender who had died so suddenly in 2009. 'Dani Jarque siempre con nosotros' ('Dani Jarque, always with us') read the message on Iniesta's T-shirt following his decisive strike against the Netherlands – proof if any were needed that football is not such an individual sport after all.

Sunday, February 9, 2014

YANGA YAICHAPA KOMOROZINE 7-0


Mrisho Ngasa (kushoto), Saimon Msuva na Didier Kavumbagu wakishangilia moja ya mabao waliyofunga leo
Wawakilishi wa Tanzania bara kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Young Africans leo imeanza vizuri mashindano hayo kwa kuibuka na ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya timu ya Komorozine de Domoni kutoka visiwa vya Comoro katika mchezo uliofanyika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Ikicheza mbele ya mashabki wake takribani elfu 17 katika Uwanja wa Taifa, kikosi cha Young Africans kiliweza kucheza vizuri na kutumia nafasi hizo ambapo imeweza kujiweka katika mazingira mazuri ya kusonga mbele katika hatua inayofuata kutokana na kuhitaji droo tu ya aina yoyote.
Mrisho Ngasa aliwainua mashabiki wa Young Africans vitini dakika ya 13 ya mchezo kufuatia kuukwamisha mpira wavuni kwa kichwa baada ya pasi ya iliyopigwa na mlinzi wa kulia Mbuyu Twite kumkuta mfungaji na kuumwamisha mpira wavuni bila makosa.
Dakika ya 20 ya mchezo, nahodha wa Young Africans Nadir Haroub "Cannavaro" aliipatia Young Africans bao la pili kwa kichwa baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na David Luhende kuunganisha moja kwa moja wavuni.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 2 - 0 Komorozine de Domoni.
Kipindi cha pili kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo Didier Kavumbagu aliiingia kuchukua nafasi ya David Luhende.
Dakika ya 58 Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao la tatu baada ya kumalizia pasi safi ya Mrisho Ngasa aliyewatoka walinzi wa Komorozine de Domoni upande wa kulia na kumpasia Kavumbagu ambaye aliukwamisha mpira wavuni.
Hamis Kiiza "Diego" aliwainua mashabiki wa Young Africans vitini dakika ya 59 ya mchezo kufuatia pasi ya Didier Kavumbagu aliywatoka walinzi wa Komorozine de Domoni. 
Mrisho Ngasa aliipatia Young Africans bao la tano dakika ya 65 ikiwa ni dakika moja baadae baada ya kazi nzuri iliyofanywa na na viungo wa Young Africans Haruna Niyonzima na Frank Domayo.
Dakika tatu baadae Mrisho Ngasa aliifungia Young Africans bao la sita na likiwa ni bao bao lake la tatu katika mchezo wa leo baada ya kumalizia mpira wa Saimon Msuva uliokoloewa na golikipa wa Komorozine.
Dakika ya 81 ya mchezo, Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao saba kufuatia kuitumia vizuri pasi ya mshambuliaji Hamis Kiiza ambapo Kavumbagu bila ajizi alimchambua mlinda mlango wa timu ya Komorozine.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 7- 0 Komorozine de Domoni.
Mchezo wa marudiano utafanyika wiki ijayo kati ya tarehe 14,15,16 Februari Visiwa vya Comoro ambapo Young Africans inahitaji sare ya aina yoyote ili kuweza kusonga mbele kutofungwa mabao zaidi ya 6-0 katika mchezo huo.
Kocha wa Young Africans Hans Van der Pluijm amesema anshukuru vijana wake wamecheza vizuri, wamepata nafasi za kufunga wamezitumia japo sio zote, kikubwa tutaendelea na mazoezi kufanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa leo.
 Young Africans: 1.Juma Kaseja 2.Mbuyu Twite, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub "Cannavaro", 5.Kelvin Yondani/Rajab Zahir, 6.Frank Domayo "Chumvi", 7.Saimon Msuva/Hassan Dilunga, 8.Haruna Niyonzima, 9.Hamis Kiiza, 10.Mrisho Ngasa, 11.David Luhende/Didier Kavumbagu