Wachezaji
watatu wanaocheza mpira wa miguu nchini Tanzania wameombewa Hati ya
Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ili wakacheze katika nchi za Thailand na
Ujerumani.
Mchezaji
Khamis Mroki Jamal aliyekuwa na timu ya Daraja la Kwanza ya Polisi Dar
es Salaam ameombewa ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Thailand (FAT) ili
akajiunge na Kabinburi ya nchini humo.
Said
Ali Nassor aliyekuwa akichezea FC Turkey ya Zanzibar na Samuel Chuonyo
wameombewa na ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) kwa ajili
ya kujiunga na klabu ya VfB Eichstatt.
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara
taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo ridhaa ya klabu zao za hapa
Tanzania itatoa ITC hizo.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
No comments:
Post a Comment