Young Africans leo itashuka dimbani kucheza na timu ya Ruvu
Shooting kutoka Mlandizi mkoani Pwani katika Uwanja wa Taifa jijini Dar
es salaam ikiwa ni sehemu ya muendelezo ya michezo ya Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania 2013/2014.
Mabingwa watetezi Yanga ina pointi 6 baada ya kucheza michezo mitano
kushinda mmoja, kutoka sare michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja
itakutana na Ruvu Shooting ambayo imejikusanyia pointi 9 baada ya
kushinda michezo mitatu na kupoteza michezo miwili.
Young Africans
ambayo leo itashuka dimbani kuhakikisha inasaka pointi 3 muhimu ili
kuweza kujiweka katika nafasi nzuri ya kuweza kutetea ubingwa wake, jana
iliendelea na mazoezi katika viwanja vya shule ya Sekondari Loyola
-Mabibo jijini Dar es salaam.
Wachezaji wote waliingia kambini
katika hosteli zilizopo makao makuu ya klabu kujiandaa na mchezo huo wa leo ambao ni muhimu kwa watoto wa Jangwani kuhakikisha wanapata
ushindi.
Kocha wa Yanga mholanzi Ernie Brandts amesema kikosi
chake kimekamilika katika kila idara kuelekea kwenye mchezo wa leo na
kusema ameyafanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika michezo
iliyopita.
Wapenzi, wanachama na washabiki wa Young Africans
mnaombwa kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa kuja kuwashangilia
vijana watakapokua wanapambana na timu ya maafande wa Ruvu Shooting.
No comments:
Post a Comment